11 March 2014

WHATEVER WENT WRONG WITH WINNIE?

He stood by his wife, still captivated, when those around him denounced her for violence and treachery. Now, even Nelson Mandela himself has come to see the truth: that he has loved not wisely but too well. John Carlin reports John Carlin Wednesday 29 March 1995 In December 1989, Nelson Mandela sent Winnie his last Christmas card from prison. "Darling, I love you," he wrote in big letters. Some months earlier he had sent her a birthday card with the message, "What a difference it makes in my life to have you". I interviewed Winnie Mandela at the end of January 1990, two weeks before her husband's release, and saw the cards on display on the mantlepiece of her home in Soweto, the place where Stompie Moeketsi had been murdered a little over a year earlier. I knew full well at the time that this was where Winnie's bodyguards, the so-called "football club", had beaten the 14-year-old boy to death. Yet, as I recall now with shame, I forgot all about Stompie the moment she entered the room. Winnie is a mountain of a woman, tall, more solid than fat, with formidable shoulders. She is old enough to be my mother. But during the 40 minutes I spent alone with her I was absolutely, helplessly beguiled. She had kept me waiting for two hours in the lounge while she performed her morning toilette. When she appeared, she glowed. She was regal and coquettish at the same time. Eyes big and bright and staring straight into mine, she purred suggestively about her impending reunion with her husband. She felt like a young bride all over again, she said. Nelson, they say, was struck like a thunderbolt the first time he saw her. He was in his late thirties, she was 20. He was married to Eveline, a sweet, soft, gentle woman who has spent the second half of her life running a grocery store in the remote little Transkei village of Comfimvaba, never remarrying. Nelson and Eveline had three children. They had been married for more than ten years the day he met Winnie. Eveline had no chance. Within months, Nelson divorced her and married Winnie. As time has shown, she was his blind spot, his fatal flaw. My eyes were opened nine months later, at the conclusion of an investigation with the BBC Radio's File on Four into the affairs of Winnie's football club. During that investigation we learnt some of the truth about Winnie. We learnt that Winnie had founded the club in 1986, ostensibly to provide amusement for unemployed young men, really to create around herself a queenly retinue that evolved over the next three years into a thuggish neighbourhood mafia. We met Dudu Chili, a neighbour of Winnie's, whose home was set on fire by the football club and whose 11-year-old niece, Finky, they shot through the head. We also met Nico Sono, who told us he had last seen his son, Lolo, battered and bleeding in the back of Winnie's van. Winnie was sitting in the passenger seat. Mr Sono pleaded with Winnie to let him go. She said: "No, he's a sell-out." That was in November 1989, more than a month before Stompie died. Mr Sono has never seen his son since. From trawling through court records, we established that members of the football club had carried out an additional 12 murders, one of them with Winnie's direct authority. We also learnt that senior members of the United Democratic Front, the African National Congress by another name before the organisation was unbanned, had a good idea of what exactly had been going on. In March 1989, they had issued a statement, led by the ANC's present secretary general, Cyril Ramaphosa, denouncing the football club's "reign of terror" in Soweto and charging that if it had not been for Mrs Mandela, Stompie would still have been alive. For a long time Winnie was Nelson Mandela's blind spot. When he could see the future of the country so clearly, he failed to see her nature. Mr Mandela himself refused to believe a word of it. Through Winnie's trial he stood by her, besotted, unpersuaded of her dark nature by the judge's verdict in May 1991 that she was guilty of kidnapping and assaulting Stompie and three others. He also refused for a long time to see that two years after his release she was carrying on an affair with Dali Mpofu, a lawyer half her age. It wasn't as if she had gone out of her way to hide what was going on. She appointed him her deputy in the ANC's social welfare department; she travelled with him to the United States, flying by Concorde from London, staying at the Beverly Hills Hotel. Early in 1992, she found out Mpofu was having an affair with another woman. It all spilled out into the open. On 17 March she wrote him a letter, later published by the Johannesburg Sunday Times. "You're running around fucking at the slightest emotional excuse," she wrote. "The fact that I haven't been speaking to Tata [Nelson Mandela] for five months now over you is no longer your concern. I keep telling you the situation is deteriorating at home. You are not bothered because you are satisfying yourself every night with a woman. I won't be your bloody fool, Dali." A month later, in April 1992, the ANC fired her from the welfare post and Mr Mandela announced that the marriage was over. Her world seemed in ruins, as it does now that President Mandela has fired her from her job as deputy minister of culture. But she bounced back. She burned with political ambition. She would not be denied the glory she believed was her due after waiting 27 years for her husband to leave jail. So she played Evita. She did what few other senior ANC leaders did: she would turn up in her Mercedes Benz to visit the poorest of the poor in the squalid squatter camps of Johannesburg and the Cape, she incited the youth with rabble-rousing speeches. Even though her fortunes fell once more in July 1993, when the ANC Women's League suspended her for displaying "defiance, insubordination and total disloyalty", she went out of her way to prove her accusers right by writing an article published in the South African press accusing the ANC leadership of rushing "with unseemly haste" to cut a deal with FW de Klerk's National Party, "to wrap themselves in the silken sheets of power". She was clever. With her populist message she tapped into a radical vein in the ANC - a small constituency but one potent enough to make it impossible for the leadership to ignore her. When President Mandela appointed his government, he made her deputy minister, guided by the same principle which had secured South Africa's successful transition to democracy: inclusivity. The coalition government, as he explained in an interview a month after his inauguration, was "full of people whose hands were dripping with blood." Why make an exception of Winnie? The logic was that once inside the government, she would toe the line. Mr Mandela made his judgement with his head, not with his heart. Despite recurrent reports in the media that the couple would reunite, the evidence suggests that now he cannot stand the sight of her. For his 75th birthday party in June 1993, he invited 650 guests. Winnie was not among them. At their daughter's wedding later that year, he turned his back on her when she approached him for a dance. Few people know what his real feelings towards her are. As a politician he is warm and generous. In his personal life, he is a sphinx. But one friend in whom occasionally he confides let slip last year that Mr Mandela had told him he could never forgive his wife. "Why not, Nelson, when you've forgiven the people who kept you in jail all those years?" the friend asked. Mr Mandela could not reply. It was again with his head and not his heart that he made the decision this week to dismiss her from his government. On the one hand, she had hardly behaved with the propriety expected of her office: during her first month in government she spent on bodyguards 40 per cent of the amount spent by the other 39 ministers and deputy ministers combined; she accepted a gift of a luxury home in Cape Town from a benefactress who, it turned out, had a diamond-smuggling conviction; she was sued in court for non- payment of a Lear-jet she hired to fly to Angola, allegedly to pick up diamonds. On the other hand, she openly criticised the government - resorting to her old populist ways - and she consistently disobeyed presidential orders. Mr Mandela calculated that the benefits of keeping her in government were now outweighed by the negative impact her scandals were having on South Africa and the world at large. He knows that she will not give up without a fight, that she may attempt to stir unrest among sectors of the black community frustrated at the government's failure to do the impossible and provide housing and jobs for all. For the long years while he was in prison she was his emotional support; he seemed her point in life. Now they are enemies and Mr Mandela's hope is that his authority will nullify her worst efforts to rekindle her ambitions. There are those who still believe that she is sincerely driven by a desire to do good not for herself, but for her people, who see her as a victim of circumstances, to be understood and therefore forgiven. They point to the burden bequeathed by her husband when he went to prison, to pursue "the struggle" while bringing up a young family alone, to her year in solitary confinement;they point to her constant harassment by the police, to her seven years of forced internal exile in the dusty little town of Brandfort, to her heroism in carrying the torch of the liberation movement during the Eighties, when all the other ANC leaders were in jail. I have had many arguments with such people. My answer is always contained in two words: "Albertina Sisulu", the wife of Walter Sisulu, who spent almost as long as Mr Mandela in prison, the mother whose sons and daughters were jailed and exiled, the politician who fought as bravely as Winnie, against odds as tough, but who remains to this day a model of kindness and moral rectitude. Mrs Sisulu and many other unsung South African heroines have suffered torments as bad as, if not far worse than, those of Mrs Mandela. Walter Sisulu is both a fortunate and a happy man. The tragedy of it all is that Mr Mandela, in the glorious winter of his years, is neither. Eyes set unflinchingly on a higher purpose, he has subdued his pain. One day, if he survives into retirement, he will look back, regret the sacrifice he has endured and ponder the thought that his life's greatest mistake was to have loved not wisely, but too well.

27 February 2013

Ayaan Hirsi Ali..

Posti yangu iliyopita niliuliza swali la kumtambua mdada kwenye picha, wengi mmepatia, ni dada Ayaan Hirsi Ali, mwanasiasa msomali aliyeamua kuipinga dini yake. Kwa habari zaidi msikilize...

....lakini kwa ufupi bado sijaielewa vizuri akili yake, sijui wenzagu mnasemaje?



19 August 2012

Da' Mija na Getrude Mongela


Licha ya kukutana na marafiki na wanablogu wenzangu, nimeweza pia kukutana na mwanamke wa shoka Mama Gertrude Mongela. Kwa kweli tulikuwa na wakati mzuri wa kuongea na kubadilishana mawazo. Nimejifunza mengi sana kutoka kwake...


10 May 2012

9 Types of intelligence.. wewe uko wapi hapo?

Wazazi na walezi, nimeileta mada hii kwenu ili kujikumbusha tu kwamba watu tumeumbwa na vipaji mbalimbali kwa hiyo hata katika watoto wetu tusiwalazimishe kusoma au kufanya mambo ambayo si kipaji chao..

  1. Naturalist Intelligence (“Nature Smart”) Designates the human ability to discriminate among living things (plants, animals) as well as sensitivity to other features of the natural world (clouds, rock configurations). This ability was clearly of value in our evolutionary past as hunters, gatherers, and farmers; it continues to be central in such roles as botanist or chef. It is also speculated that much of our consumer society exploits the naturalist intelligences, which can be mobilized in the discrimination among cars, sneakers, kinds of makeup, and the like.


 2. Musical Intelligence (“Musical Smart”) Musical intelligence is the capacity to discern pitch, rhythm, timbre, and tone. This intelligence enables us to recognize, create, reproduce, and reflect on music, as demonstrated by composers, conductors, musicians, vocalist, and sensitive listeners. Interestingly, there is often an affective connection between music and the emotions; and mathematical and musical intelligences may share common thinking processes. Young adults with this kind of intelligence are usually singing or drumming to themselves. They are usually quite aware of sounds others may miss.

  
3. Logical-Mathematical Intelligence (Number/Reasoning Smart) Logical-mathematical intelligence is the ability to calculate, quantify, consider propositions and hypotheses, and carry out complete mathematical operations. It enables us to perceive relationships and connections and to use abstract, symbolic thought; sequential reasoning skills; and inductive and deductive thinking patterns. Logical intelligence is usually well developed in mathematicians, scientists, and detectives. Young adults with lots of logical intelligence are interested in patterns, categories, and relationships. They are drawn to arithmetic problems, strategy games and experiments.
  

4. Existential Intelligence Sensitivity and capacity to tackle deep questions about human existence, such as the meaning of life, why do we die, and how did we get here.


 5. Interpersonal Intelligence (People Smart”) Interpersonal intelligence is the ability to understand and interact effectively with others. It involves effective verbal and nonverbal communication, the ability to note distinctions among others, sensitivity to the moods and temperaments of others, and the ability to entertain multiple perspectives. Teachers, social workers, actors, and politicians all exhibit interpersonal intelligence. Young adults with this kind of intelligence are leaders among their peers, are good at communicating, and seem to understand others’ feelings and motives.


 6. Bodily-Kinesthetic Intelligence (“Body Smart”) Bodily kinesthetic intelligence is the capacity to manipulate objects and use a variety of physical skills. This intelligence also involves a sense of timing and the perfection of skills through mind–body union. Athletes, dancers, surgeons, and craftspeople exhibit well-developed bodily kinesthetic intelligence.
  

7. Linguistic Intelligence (Word Smart) Linguistic intelligence is the ability to think in words and to use language to express and appreciate complex meanings. Linguistic intelligence allows us to understand the order and meaning of words and to apply meta-linguistic skills to reflect on our use of language. Linguistic intelligence is the most widely shared human competence and is evident in poets, novelists, journalists, and effective public speakers. Young adults with this kind of intelligence enjoy writing, reading, telling stories or doing crossword puzzles.
  

8. Intra-personal Intelligence (Self Smart”) Intra-personal intelligence is the capacity to understand oneself and one’s thoughts and feelings, and to use such knowledge in planning and directioning one’s life. Intra-personal intelligence involves not only an appreciation of the self, but also of the human condition. It is evident in psychologist, spiritual leaders, and philosophers. These young adults may be shy. They are very aware of their own feelings and are self-motivated.

  
9. Spatial Intelligence (“Picture Smart”) Spatial intelligence is the ability to think in three dimensions. Core capacities include mental imagery, spatial reasoning, image manipulation, graphic and artistic skills, and an active imagination. Sailors, pilots, sculptors, painters, and architects all exhibit spatial intelligence. Young adults with this kind of intelligence may be fascinated with mazes or jigsaw puzzles, or spend free time drawing or daydreaming.

Elimu yote ni kwa hisani ya  Bwana, Howard Gardner na unaweza kuipata hapa.

23 November 2010

Kazi ya mikono yangu wiki hii....!! Kutoka kwa Da' Mija.

01 October 2007

Malkia Nzinga Mbande wa Angola.


Nikiwa katika harakati ya kukusanya habari za wanawake waliotia fora duniani, nimeona niirudishe habari hii niliyoiandika hapo nyuma 2005 wakati nikianza kublogu hii ni kuwapa fursa wale ambao hawakuweza kuisoma nao wapate kumfahamu mama huyu, haya endelea...

Kama ukibahatika sasa hivi kukutana na Mreno, wewe jifanye kama unamchokoza juu ya wanawake wa afrika kwamba hawana lolote na hawawezi lolote, uone atakavyokushangaa, na bila shaka atakutupia swali kwamba unaishi dunia gani wewe?

Wasomaji msishangae, kwani aisifiae mvua...imemnyea. Hii yote imetokana na mwanamke mmoja jasiri, shupavu, mwenye akili sana na asiyetaka kuonewa wala kudharauliwa, si mwingine ni Malkia Nzinga Mbande. Mwanamama huyu aliyezaliwa mwaka 1583 na kufa 1663, alikuwa ni mtoto wa chifu na aliishi kipindi ambacho biashara ya utumwa ndio ilikuwa imepamba moto kwelikweli, kwa bahati mbaya baba yake alifariki na hivyo kaka yake mkubwa bwana Ngola Ngoli Mbandi akarithishwa madaraka ya baba yake. Mm! kaka huyu bila shaka aliguna kwa kujua kabisa kasheshe analotakiwa alikabili la kuwazuia wareno kuingia nchini kwao, lakini afanyeje na yeye ndio mwanaume na kama inavyojulikana kwa wengi mwanaume anaweza kila kitu na daima si mwoga, ikabidi ayavae madaraka huku akijua kabisa yeye ubavu wa kukabiliana na wareno hana na ni
mwoga kufa.

Dada yake, Nzinga baada ya kuona kaka yake anasua-sua ikabidi amwambie, kaka ni lazima uchukue hatua juu watu hawa na kuwazuia kuingia kututawala, lakini kwa vile kaka yake alikuwa mwoga ikabidi amwombe dada yake amsaidie, mara moja bila kuchelewa mwana mama Nzinga akaanza kuchukua hatua za utekelezaji na akafanikiwa kuwashawishi wareno katika kuandika mkataba wa makubaliano ya amani.

Tarehe ikapangwa ya kuweka saini makubaliano hayo, Kaka mtu kwa woga akakataa kwenda hivyo ikabidi Nzinga amwakilishe, akaenda na watumishi kadhaa lakini walipofika ndani ya ukumbi Nzinga akagundua kwamba hakuwekewa kiti yeye kama kiongozi wa nchi yake isipokuwa gavana wakireno peke yake, mwanamama akaona dharau gani hii? mara moja akapiga kofi na mmoja wa watumishi wake akaja mbele yake na kuinama magoti na mikono chini, Nzinga akakaa juu yake, kwa hiyo suala la gavana kukaa kwenye kiti peke yake likawa ngoma droo. Gavana akamtizama yule mama bila kummaliza na kubaki na aibu ya kuzidiwa maarifa tena na mwanamke, bila shaka alibaki akijiambia duh! kumbe wanawake nao wamo!!!

Nzinga baada ya kugundua kwamba kaka yake si kiongozi mzuri na hawezi kila kitu, alimfunga na kujitangaza kwamba yeye ndiye atakayeshika nchi kinyume na desturi ya nchi yao kwamba mwanamke haruhusiwi kushika wadhifa wowote wa uongozi katika serikali, minong'ono ya hapa na pale ilitokea lakini haikufika mbali kwani Nzinga alithibitisha ujasiri wake kwa vitendo. Na ni hapo ndipo umalkia wake ulipoanzia.

Kwa muda wa miaka arobaini ya uongozi wake, wareno walishindwa kuitwaa Angola hadi alipofariki, mwanamama huyu alijulikana na kuogopwa sana na ulaya nzima kwa mbinu zake thabiti za kijeshi, alijulikana kama mwanamke mpiganaji, jasiri na mwenye akili.
Hebu fikiria wareno, pamoja na kuwa na silaha imara na za kisasa ukilinganisha na za Malkia Nzinga, lakini walishindwa kuiteka Angola hadi Malkia Nzinga alipokufa.

Huyu kweli ni mwanamke wa shoka, na nina amini kila mwanamke anaweza kuwa mwanamke wa shoka, pale atakapoamua kufanya jambo kwa moyo na kuondoa uwoga. Hapa duniani kila jambo linawezekana, tatizo liko kwetu sisi wenyewe kutanguliza woga na kutokutaka kusumbuka.

16 March 2007

Miriam Makeba

Miriam Makeba ni mwanamuziki mashuhuri sana na mwanaharakati kutoka Afrika kusini. Alizaliwa 04-03-1932 Johannesburg. Baba yake Caswell Mpambane Makeba alikuwa ni kabila la xhosa na Mama yake Christina Nomkomendelo Jele alikuwa ni mswazi.

Miriam ni mtoto wa sita na wa mwisho kwa mama yake, na wa kwanza na wa mwisho kwa baba yake. Mama yake aliolewa na Makeba baada ya ndoa yake ya kwanza na bwana Mahlangu kuvunjika wakiwa tayari na watoto watano ambao ni, Joseph, Hilda, Mizpah, Ethel na mmoja aliyefariki akiwa mchanga.

Familia yao ilikuwa ni masikini sana. Baba yake ambaye alikuwa ni mwalimu kitaaluma hakuwa na kazi yoyote, kwani katika kipindi hicho cha utawala wa kikaburu ilikuwa ni ngumu sana kwa mwalimu mwafrika kupata shule ya kufundisha. Mama yake alikuwa anafanya kazi za ndani kwa wazungu na wakati mwingine kuuza pombe ya kienyeji(umqombothi) ili kuihudumia familia. Wakati huo ilikuwa ni kinyume cha sheria kwa mwafrika kunywa au kutengeneza pombe ya aina yoyote ile lakini hata hivyo ilikuwa ikitengenezwa na kunywewa kwa kificho. Kutokana na hali hiyo polisi wa kizungu walikuwa wakivamia mara kwa mara makazi ya waafrika ili kuwakamata wasiotii amri hiyo ya kunywa na kutengeneza pombe. Ilikuwa ni pale Miriam alipofikisha umri wa siku 18 tu tangu azaliwe, polisi walivamia maeneo ya waafrika na kufanikiwa kumkamata mama Miriam akiuza pombe, bila huruma wala kujali kwamba ana mtoto mchanga walimbeba hadi mahakamani na kuhukumiwa adhabu ya kifungo cha miezi sita jela. Hakuwa na jinsi ya kumuacha Miriam, alimbeba Miriamu wake na kwa pamoja kukaa jela kwa miezi sita. Hivyo basi Miriam akiwa katika umri mdogo kabisa aliweza kuionja jela.

Walipotoka Jela walikuta baba (Makeba) amepata kazi katika kituo cha kuuza mafuta cha Shell, hivyo maisha yao yakawa na nafuu. Maisha yaliendelea vizuri hadi mwaka 1938 ambapo Mzee Makeba alifariki dunia, Miriam akiwa na umri wa miaka 6. Taabu ikarudi palepale, na kwa vile kipato cha mama yao hakikuweza kutimiza mahitaji ya watoto wote sita, ikabidi ahamishie watoto wake kijijini kwa bibi yao aliyeitwa MaVilakazi, (huyu ni mama mzazi wa mama yake na Miriam). Na yeye akabaki mjini kwa ajili ya kazi. Miriam anasema kuanzia hapo ilikuwa si rahisi kuonana na mama yake, muda mwingi alikuwa kazini mjini na kwa vile Miriam alikuwa bado ni mdogo na anayehitaji uwepo wa mama yake zaidi, ilibidi awe anafunga safari ya mjini kila mwisho wa juma baada ya masomo kwenda kumuona mama yake aliyekuwa akikaa kwa wazungu aliokuwa akiwafanyia kazi.



Upande wa pili kwa bibi MaVilakazi, familia ilikuwa ni kubwa ya wajukuu 21,(watoto wengine ni wa kaka na dada za mama yake na Miriam). na yenye kipato kidogo, siku nyingine walikula na siku nyingine walilala njaa, lakini maisha yalikuwa yakienda. Miriam anasema kwamba pamoja na hali ile duni pale kwa bibi yake, bibi yake hakuwa na mzaha kabisa na kanisani, kila jumapili ni lazima kwenda kusali utake usitake. Miriam hakupenda sana kutokana na vile bibi yao alivyokuwa akitunza hela na vitu vingi vizuri kwa ajili ya kutoa sadaka wakati nyumbani wanalala na njaa. Wakati mwingine Padri wao aliwapita njiani wakati wa mvua wakinyeshewa bila kutoa hata lifti kwa gari ambalo limenunuliwa kwa sadaka zao. Miriam anasema kitu kimoja kilichomfanya asiache kwenda kanisani kilikuwa ni uimbaji tu, alipenda sana kuimba, na kanisani waliimba sana. Baada ya miaka kupita, mama yake alianza kuchoka na kuugua ugua, lakini alishindwa kuacha kazi kwa vile alikuwa akimsomesha Miriam ambaye ndio alikuwa ameanza chuo, Miriam naye alikuwa amechoka na maisha duni waliyokuwa wakiishi, maisha ya kuvaa 'kauka nikuvae' hali hii pamoja na kuona mama yake akiugua kila mara ikamfanya kufikia uamuzi wa kuacha shule na kutafuta kazi. Alipata kazi yake ya kwanza ya kuangalia mtoto katika familia ya kigiriki, alihamia pale na ulipofika mwisho wa mwezi wa kwanza alilipwa mshahara wake vizuri, mwezi uliofuatia akaambiwa asubiri kidogo kwa vile mwajiri wake alikuwa na matatizo kidogo, mwezi wa tatu mke wa mwajiri wake akamsingizia ameiba vitu ndani kwa hiyo hakuna mshahara. Miriam akaona huu ni uendawazimu, akaamua kuacha kazi. Akapata kazi nyingine kwa wazungu hii nayo ni ya kuangalia mtoto, anasema mambo yalienda vizuri hadi siku moja wakati wa likizo ambapo walisafiri, wakiwa huko wakafikia hoteli ya ufukweni. Hivyo wakati wa jua wao walikuwa wakijianika mchangani na Miriam akapewa kazi ya kukusanya shells kwa ajili ya kazi za sanaa za yule mzungu alizokuwa akizifanya. Siku ya kuondoka ilipofika bila sababu maalumu Miriam akaambiwa apande treni arudi, na wao wakarudi na gari walilojia. Katika ukusanyaji wake zile sheli aliweza kujaza ndoo mbili, hizi nazo aliambiwa arudi nazo kwa treni. Kwa hiyo yeye, mabegi yake na ndoo mbili zilizojaa shells tena katika daraja la tatu la treni!! hakuwa na la kufanya akapanda na kuanza safari ya kurudi, wakiwa njiani wakaambiwa inabidi wabadili treni wakatelemka na kusubiri nyingine. Ilipokuja akaanza kupandisha begi lake la nguo, akachukua ndoo ya kwanza ya shells, alipotaka kuchukua ya pili treni ikaanza kuondoka, haraka haraka akarukia ndani ya treni bila ndoo ya pili. Akaitizama ile ndoo iliyobakia akasema 'katu siiachi hii treni kwa ajili ya hiyo ndoo ya shells, sina hela nyingine ya nauli na hii treni ikiniacha ndiyo itakuwa mbaya zaidi'. Treni ikazidi kukaza mwendo na yeye akazidi kuitizama ile ndoo inavyobakia. Kufika Johannesburg alikuwa akitetemeka kwa hofu, alijiuliza atamwambia nini mwajiri wake kuhusu ndoo ya pili? baada ya kufikiri akaamua hatorudi tena kazini, hivyo akaachana na kazi ile nakuamua kurudi nyumbani.




Huku nyumbani hali ya mama yake ilizidi kuwa mbaya, miguu yake ilianza kuvimba hadi kushindwa kutembea, walimpeleka karibu kila hospitali bila mafanikio. Hivyo wakaamua kumpeleka kwa mganga wa kienyeji 'isangoma', kule wakaambiwa kwamba kuumwa kwake si bure, mizimu ya kwao imemchagua awe mganga wa kienyeji 'isangoma' ili aweze kuwasiliana nao moja kwa moja na kuwaeleza watu mambo yaliyopita, kutabiri yajayo na pia kutibu wengine. Na kama anataka kupona maradhi yanayomsumbua ni lazima akubaliane na hilo, wote walifurahi na kukubali kwani wanasema kuchaguliwa na mizimu ilikuwa ni kama zawadi. Baada ya kukubali alitakiwa kufuata mchakato wa Ukutwasa. Ukutwasa ni mchakato au hatua za kumfanya mtu kupokea nguvu za mizimu hadi kuweza kuponya wengine (Mganga). Aliondoka na kwenda Swaziland ambako ukutwasa wake ulikuwa unafanyikia. Kutokuwepo kwa mama yake nyumbani kulimfanya yeye kuchukua majukumu ya mama yake, kama kuilisha na kuiangalia familia kwa ujumla. Kwa jukumu hili ilibidi atafute kazi tena na safari hii akaamua kuwa dobi. Wakati huo kulikuwa na wafanyakazi wengi wageni waliokuwa wakifanya kazi nchini, na hao ndio walikuwa wateja wake, kila jumatatu alikwenda kukusanya nguo zao chafu na ijumaa kuwarudishia safi. Haya ndiyo yakawa maisha ya Miriam.




Tangu akiwa shule hadi kipindi hiki anachofanya kazi za udobi, Miriam alikuwa na mpenzi wake chotara aliyeitwa James Kubayi au Gooli kama alivyojulikana kwa marafiki zake. Urafiki wao ulikuwa mzuri sana na kila mara walikuwa wote, Gooli alikuwa pamoja naye alipoacha shule, alipopata kazi kwa wazungu na hata sasa wakati mama yake alipokuwa Swaziland. Miriam alimpenda na kumuamini sana kiasi kwamba haukupita muda akapata ujauzito, hapo akiwa na umri wa miaka 17 tu. Anasema alikuwa na bahati sana kwani Gooli hakumtelekeza, alimchukua kumuhamishia nyumbani kwao. Familia ya kina Gooli ilikuwa inajiweza kidogo, mama yake alikuwa akipika pombe kama biashara ya ziada. Akiwa katika familia ya wakwe na mimba mambo yalikuwa magumu kidogo kwani Gooli hakuwepo muda mwingi alikuwa anachukua mafunzo ya upolisi katika mji mwingine hivyo alikuja pale kusalimia tu. Muda wa kujifungua ulipofika alipelekwa hospitali na kujifungua mtoto wa kike aliyemwita Sibongile au kwa kifupi Bongi. Alipotoka hospitali maisha hayakuwa rahisi tena, kazi zote za pale kwa mkwewe alitakiwa azifanye yeye, alikuwa akiamka saa 10 alfajiri kumuosha na kumlisha Bongi, kupika chakula cha wengine na kufanya shughuli zote za ndani na bado Bongi akilala alibaki kuhudumia wateja wa pombe hadi usiku wa manane.




Gooli alimaliza mafunzo yake na kurudi nyumbani, lakini alikuwa amebadilika sana tabia, alikuwa mkorofi na mwenye wivu wa kupindukia, alianza tabia ya kumpiga Miriam bila sababu za msingi, Miriam hakuwa na haki ya kusema lolote kwa Gooli, Miriam alianza kusononeka lakini alivumilia, alijua Gooli hampendi tena lakini hakujua ni kwa kiasi gani hadi siku moja alipomfumania na ndugu yake. Miriam alijua amemfumania mumewe kwa hiyo hapo ana nguvu ya kusema lakini badala yake kibano kilimgeukia yeye na kupigwa kipigo cha kifo. Kuanzia hapo alisema imetosha, alimchukua mtoto wake akakodi taksi na kurudi nyumbani kwao bila kuaga. Gooli alimfuata kumrudisha lakini alikuta mama yake amesharudi toka Swazilandi, alimkurupua vibaya sana na toka siku hiyo hakurudi tena na ndiyo ukawa mwisho wa Miriamu na baba mtoto wake kuonana.




Miriam sasa akiishi kwa mama yake, hakuwa na kazi yoyote ya kipato zaidi ya kumsaidia mama yake shughuli za Usangoma. Mama yake akaona hali hii haitamfikisha mahali popote mwanae, akamwambia ni lazima abadilishe kabisa mwelekeo wa maisha yake kwa kutafuta kitu cha kufanya. Miriam akaona ni bora aende mjini akaangalie cha kufanya, akamuacha Bongi na mama yake yeye akaenda mjini Johannesburg.





Johannesburg alifikia kwa binamu yake aliyeitwa Sonti Ngwenya, Sonti alikuwa na mwanaye wa kiume aliyeitwa Zweli ambaye walikuwa karibu rika moja na Miriam. Zweli na baadhi ya marafiki zake walikuwa wameanzisha bendi ya muziki iliyoitwa Cuban Brothers, wote walijua Miriam anaweza kuimba hivyo siku moja wakamuomba kama atataka kujiunga na bendi yao, Miriam akaona hii itakuwa ni kichekesho lakini akakubali kwa vile alikuwa tayari kufanya jambo jipya katika maisha yake. Akiwa Cuban Brothers walifanya maonyesho sehemu mbalimbali kama makanisani, kwenye sherehe za kuchangisha fedha (fundraising) na sehemu nyingine nyingi. Katika kipindi hicho kulikuwa na ukumbi maarufu sana uliojulikana kama Donaldson Community Centre ambao Cuban Brothers mara nyingi walikuwa wakipiga muziki hapo, huu ni ukumbi ambao watu wengi maarufu na wasio maarufu walipenda kwenda. Siku moja wakiwa katika onyesho Miriam alinong'onezwa na mwenziye kwamba Manhattan brothers wako ndani ya nyumba. Manhattan Brothers band kilikuwa ni kikundi cha muziki kinachojulikana sana wakati huo, kila mtu alipenda muziki wake. Baada ya onyesho Miriam alifuatwa na kijana mmoja na kujitambulisha kwa jina la Nathan Mdledle na kuwa ni kiongozi wa kundi la Manhattan Brothers, Miriam hakuamini macho yake kwamba anaongea na Manhattan brother, wakati akishangaa Nathan akamwambia anapenda jinsi anavyoimba, kama hiyo haikutosha, Miriam anasema almanusura aanguke baada ya kuambiwa anaonaje kama anataka kufanya usaili wa kujiunga na Manhattan brothers. Alikwenda kufanya usaili na kushinda hivyo akapata kazi.



Akiwa na Manhattan brothers aliweza kujulikana sana, hii ni kwa sababu kundi hili lilikuwa na kazi nyingi za ndani na nje ya nchi. Anasema Manhattan ilimfungulia milango yake ya mafanikio kwani baada ya kuwa nao makundi mengine mengi yalianza kumfuata ili afanye nao kazi yeye binafsi kama Miriam. Mwaka 1958 alipata bahati nyingine ya kuombwa kujiunga na kikundi cha African Jazz and variety. Hiki kilikuwa ni kikundi kinachozunguka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi. Mwanzilishi wake alikuwa ni mama wa kiyahudi aliyeitwa Sara Silvia. Mama huyu alisema kuwa atahakikisha African Jazz and variet, inakuwa ni kikundi cha kwanza ambacho waafrika wataruhusikwa kupiga muziki mbele ya wazungu. Na kweli ndivyo ilivyokuwa, kikundi hiki kilikuwa kikifanya onyesho kwa wazungu watupu kila Alhamisi katika ukumbi wa Johannesburg city. Mwaka 1959 akiwa bado na African Jazz, alipata bahati nyingine kubwa ambayo tunaweza kusema ndiyo iliyo mtoa. Mtengeneza filamu mmoja kutoka Marekani aliyeitwa Lionel Rogosin, alimuona Miriam akiimba kwenye shoo za African jazz, alipenda sana uimbaji wake na akamuomba aimbe katika filamu aliyokuwa akiitengeneza COME BACK AFRICA. Miriam alikubali na akaigiza na kuimba katika filamu ile. Baada ya hapo Lionel Rogosin aliondoka na kuwaahidi kuwataarifu atakapomaliza kuitayarisha filamu ile. Huku nyuma mwaka huo huo 1959 februari, bahati nyingine ikaja kwa Miriam, King Kong Jazz Opera ilifunguliwa na Miriam akapata nafasi ya kuimba na kuigiza mle kama Joyce "Queen of Back of the Moon".

KUONDOKA AFRIKA.

Baada ya muda kupita Lionel Rogosin akaleta habari kwamba filamu yake ya COME BACK AFRICA imekamilika na imepokelewa vizuri hivyo ameiingiza katika Tamasha la Filamu la venice Italia(VENICE FILM FESTIVAL) kwa hiyo anamualika Miriamu Makeba kuungana naye katika kuitambulisha film hiyo huko Venice na Ulaya kote.

Anasema hakuamini macho yake kupata nafasi ya kwenda Ulaya, wakati huo kazi yake ilikuwa ikienda vizuri sana alikuwa bado akifanya kazi na King Kong kitu ambacho ni hatua kubwa sana kwake yeye na sasa anapata nafasi ya kwenda Ulaya? Hakuamini macho yake. Haraka aliomba pasipoti, alisumbuliwa sana hadi kuipata kwa sababu makaburu walijua kila kitu kuhusu Miriam na walijua kwamba ameshiriki katika filamu ya come back Africa, hatimaye alipewa na kuondoka bila kuchelewa, ilikuwa ni mwaka 1959.



Safari yake ilianza na alifika London salama na kukutana na mwenyeji wake Lionel Rogosin na mkewe. Akiwa pamoja na wenyeji wake sasa walianza safari ya kuelekea Venice Italy kwa gari. Walifika Venice wakazindua film yao katika tamasha lile na kwa bahati film yao ikawa ni miongozi mwa film zilizopata tuzo, ilishinda Critic Award.



19 November 2006

Shabiki na Ushabiki!

Wasomaji wapendwa, habari hii chini inawajia kwa hisani ya mwanablogu MtiMkubwa.....

Naam,

Hakuna kitu kibaya kama unazi, ushabiki, au umaamuma. Ushabiki unaweza kuwa wa kidini, kiitikadi, kikabila, kirangi, kimichezo, kitaaluma au hata kumshabikia mtu binafsi. Shabiki akiamua kushabikia jambo analoshabikia hata wakitumwa malaika, mitume na manabii kumsilimu hasilimiki.

Siku chache zilizopita nilikutana na shabiki mmoja. Huyo shabiki alipoanza ushabiki wake nilifikiri alikuwa anatania kwa sababu sijawahi kukutana na mtu anayemshabikia mtu kwa namna ya yule shabiki. Sina jinsi ya kumuelezea shabiki mwenyewe lakini ni kijana anayetokea mikoa ya kanda ya ziwa, tena ana lafudhi kali ya kanda ya ziwa, na aliyebahatika kupata ajira serikalini. Tulikuwa tunazungumzia operesheni bomoa bomoa ya RC Kandoro, ndipo huyo shabiki alipoingilia mazungumzo na kusema "..Hiyo yote ni mipango ya JK..Unajua ameunda Wizara ya Mazingira iri kumekishua kwamba jiji rinakuwa safi..Yeye mwenyewe yuko Marekani rakini huku nyuma kaacha maagizo akirudi Wamachinga wawe wameshaondoka.." Miye na jamaa yangu mwingine tukageuka kumsikiliza shabiki. Alipoona tumeonyesha nia ya kumsikiliza ikawa tumefungulia ushabiki "..JK bwana ni mjanja sana. Unajua kamreta huyu kocha iri Tanzania iende woridikapu. Na huo ni mmoja wa mipango yake ya muda mrefu..Na utaona Tanzania itafika woridikapu.." Jamaa yangu akamuuliza "..Tanzania itafika woldikapu kwa sababu ya JK?.." Yule kijana akajibu "..Usifanye mchezo na JK, nyie turieni mtaona..Unajua JK amekwenda Marekani kwenye jenero asembri rakini pia kaenda kuonana na Bush..Yaani Bush anamuadimaya sana JK katika viongozi wote wa Afrika..." Jamaa yangu akaniambia "..Unasikia insaidi storizi hizo?.." Nikamjibu "..Nazisikia.." Yule kijana kusikia hivyo moto ukazidi kumpanda "..Kwa mikakati ya JK bai dhe endi ofu dhisi manthi yaani Septemba umeme utakuwa umerudi nchi nzima..Yaani jamaa anachapa kazi siyo mchezo endi hi izi so krozi tu dhe pipo kwa hiyo anayajua matatizo ya Watanzania kwa karibu zaidi anraiki Mkapa..Mkapa arikubarika inteneshinari rakini rokari hakuwa karibu na wananchi..JK ameshaanza kurudisha njia za kuu uchumi mikononi mwa wananchi, ATC tayari imesharudi harafu sasa hivi anashugurikia mikataba ya madini, yaani kwa kweri katika kipindi kifupi amefanya mambo mengi sana tena makubwa.." Jamaa yangu akamwambia "..Aisee.." Hapo shabiki ndiyo akazidi kupamba moto "..Ingekuwa JK ndiye ariyekuwepo madarakani wakati ure Baba wa Taifa asingefariki.." Niliposikia hivyo ikabidi niingilie mazungumzo "..Hebu tuache ushabiki hapa na tuzungumze yaliyo kweli..Ni kweli kuwepo kwa JK madarakani kunaweza kurefusha au kufupisha maisha ya mtu au watu.." Kabla sijamaliza hoja yangu yule shabiki akarukia "..Na ndiyo maana awamu ya ine sera yao ni Maisha bora kwa Watanzania wote..JK anataka kira Mtanzania awe na maisha bora..Ndiyo maana hapati usingizi kwa kufikiri jinsi gani atawapatia Watanzania maisha bora..Yaani kwa kweri tunaomjua kwa karibu tunaerewa anavyohangaika kuwatafutia Watanzania maisha bora.." Jamaa yangu akamwambia "..Ndiyo hatamu na maana ya uRais kulinda masilahi ya wananchi wake.." Shabiki akajibu "..Rakini siyo maraisi wote wanakumbuka hiro na hapo ndipo JK anapochukua pointi kurinda masirahi ya wananchi..JK bwanaa..Yaani wee acha tu..Baadhi ya watu hawamuerewi kwa hiyo wanamkritisaizi widhiauti eni graundis..Aripoteuwa kabineti wapinzani wakamkritisaizi eti baraza kubwa sana.. Yeye ariunda kebineti kubwa iri kuzidisha efishensi..Sasa hivi ware wariomkritisaizi wameshushuka baada ya kuona jinsi kabineti inavyochapa kazi..Ini Tanzanian histori kabineti hii ni drimu timu..Hakuna kabineti iriyowahi kuundwa kama hii ya sasa hivi, yaani kira ariyepewa wizara inamfiti..Teri mi huu izi ini dhe rongi ministri?! Shemeji yangu Dokta Migiro fits pafektri weri in foreni afeazi.. Mama Meghji -fainansi, bajeti aliyoisoma hata Kenya na Uganda wameomba kopi..Msabaha kwenye madini na nishati humo ndiyo mwake kabisa, unajua mambo ya madini ni grobo biznesi na Msabaha ni mtu dipromasia kwa hiyo atayauza madini kiurahisi na kwa bei nzuri tu...Mramba wizara ya miundombinu, jamaa ni rongi eksipiriensid na JK kamuweka pare makusudi kwa sababu pare panatakiwa mtu mwenye rongi eksipiriensi.." Jamaa yangu akamwambia "..Ahaaa hili baraza kiboko.." Shabiki akarukia "..Harafu ormosti dhe whori kabine au thrii kota ni niyuu fesiz tena ni vijana vijana na akina mama kawapa wizara nyeti zote isipokuwa urinzi..Hapo ndipo anapothibitisha Nguvu mpya, Ari mpya, na Kasi mpya JK bwana ni kiboko..Nyie bwana JK izi dhe prezidenti..Halafu amekubarika na wananchi, ukiangaria historia ya Tanzania ni viongozi wanne tu wariokubarika na Wananchi; Hayati Baba wa Taifa, Hayati Sokoine, Agostini Murema, na JK! Bati Murema disapointedi dhe masizi kwa hiyo femu yake inawitha siku hadi siku.." Wakati anaendelea kutupiga darasa kilongalonga chake kikamuita akasogea pembeni kuongea, alipomaliza akarudi kutuomba radhi kwamba ameitwa ofisini, akaondoka. Miye na Jamaa yangu tukaondoka tukiwa ndani ya gari jamaa yangu akaniambia hayo ndiyo maoni ya wengi.

Leo nimekutana na kipande kingine cha habari. Miye nimekiona kama ushabiki wa yule shabiki wa Kikerewe. Ningelikuwa na namna ningewaomba viongozi wambane huyo tarishi wa Waziri Mkuu wa Malaysia aliyeko nchini Tanzania juu ya mkataba wa IPTL. Halafu pia kumdhibiti asije akatuletea balaa nyingine kubwa zaidi ya IPTL. Ushabiki wenyewe huo hapo chini.

Ziara za JK nje zaanza kuzaa matunda 2006-11-18 10:34:26 Na Joseph Mwendapole

Ziara za Rais Jakaya Kikwete nje ya nchi kutafuta wawekezaji, sasa zimeanza kuzaa matunda kutokana na baadhi ya wawekezaji kuwasili nchini kuangalia mazingira ya uwekezaji. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Waziri wa Mipango na Uwezeshaji, Dk. Juma Ngasongwa, alisema makampuni mengi yamekuwa yakiandika barua pepe yakionyesha nia ya kuja kuwekeza nchini. Alitaja baadhi ya wawekezaji ambao tayari wamewasili nchini kuwa ni Benki ya Uwekezaji ya Kuwait, ambayo Mkurugenzi wake, Bw. Jassem Zainal yuko nchini kuangalia mazingira ya kuwekeza. Waziri Ngasongwa alimtaja mwingine kuwa ni Naibu Waziri Mkuu wa Malaysia, Bw. Annuary Ibrahim, ambaye ameambatana na wageni hao. Alisema Bw. Ibrahim aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete, kusaidia kampeni zake za kutafuta wawekezaji wa kuja kuwekeza nchini. Dk. Ngasongwa alisema Bw Ibrahim ni rafiki wa kweli aliyekubali ombi la Rais Kikwete kuitangaza Tanzania duniani. ”Kuonyesha kuwa kweli ni rafiki yetu, Bw. Ibrahim leo ametuletea wawekezaji watakaowekeza kwa kiasi kikubwa katika sekta ya fedha,” alisema. Alisema wawekezaji hao bado wanaendelea na mazungumzo na serikali ili kuangalia namna ya kuendesha shughuli zao. ”Wamenihakikishia kuwa, mambo yakienda sawa mwanzoni mwa mwaka ujao wataanzisha benki kubwa ambayo itakopesha watu wengi kwa riba ndogo,” alisema Dk. Ngasongwa. Dk. Ngasongwa alisema Korea imeahidi kujenga daraja la Malagarasi kwa dola milioni 25 za Kimarekani ambazo zitatolewa kwa Tanzania kama mikopo nafuu. Alisema wawekezaji wa kampuni ya Samsung na DAEWOO, imeahidi kuwekeza upande wa teknolojia ya habari na mawasiliano. Alisema serikali ya nchi hiyo pia imekubali kuwekeza katika uzalishaji wa nishati ya umeme. Akizungumzia ziara ya China, Dk. Ngasongwa alisema serikali ya nchi hiyo imeahidi kusaidia kuongeza uzalishaji katika mradi wa Kiwira hadi kufikia Megawat 200 kutoka sita za awali.

04 November 2006

Huyu ni nani?

22 October 2006

Wangari Muta Maathai.


Wangari Muta Maathai, mwanamke mwafrika wa kwanza kushinda Nishani ya amani ya Nobel tangu kuanzishwa kwake mwaka 1900.

Mwaka 2004, niliposikia mwanamazingira mama mpanda miti, Wangari Maathai ndiye mshindi wa nishani ya Amani ya nobel, nilishindwa kabisa kuelewa ni kwa kigezo gani aliweza kuchaguliwa kuwa mshindi wa tuzo hii ambayo ni moja wapo ya tuzo ya zaidi ulimwenguni. Nilijiuliza "Miti na Amani" wapi na wapi? na kutokana na swali hilo nilianza kumfuatilia kwa makini zaidi mama huyu na ndipo nilipogundua uwezo mkubwa wa akili alionao mama huyu.

Mama Wangari Muta Maathai alizaliwa 01/04/1940 katika kijiji cha Tetu kilichopo Nyeri nchini Kenya. Baba yake bwana Muta Wanjugu na mama yake Lydia Wanjiru Muta ambao walikuwa wakulima, walimpeleka Wangari shule baada ya kaka mkubwa wa Wangari Nderitu kushauri kwamba dada yake ni lazima asome kitu ambacho katika miaka hiyo kilikuwa ni nadra sana, ni watoto wachache sana wa kike walipelekwa shule katika miaka hiyo.

Hivyo alianza shule ya msingi Itithe mwaka 1948 hadi 1951 darasa la kwanza hadi la nne. Akafuatia shule ya Mtakatifu Cecilia mwaka 1952 hadi 1955 darasa la tano hadi la nane. Alimaliza elimu ya msingi na kujiunga na sekondari ya wasichana ya Loreto kidato cha kwanza hadi cha nne kati ya mwaka 1956 na 1959. Baada ya hapo alibahatika kupata ufadhili wa kwenda nchini Marekani kwa ajili ya masomo ya juu zaidi, huko alijiunga na chuo cha Mtakatifu Scholastica cha Kansas kwa Shahada yake ya kwanza katika baiolojia ikiwa ni mwaka 1960 hadi 1964, mwaka huo huo 1964 alijiunga na chuo kikuu cha Pittsburgh kwa shahada ya pili ambapo alimaliza mwaka 1965. Mwaka 1966 alirudi nyumbani Kenya na kupata kazi katika Chuo kikuu cha Nairobi kama mtafiti msaidizi.

Mwaka 1969 alifunga ndoa na mfanyabiashara na mwanasiasa Bwana Mwangi Mathai, ambapo walibarikiwa kupata watoto watatu, Wanjira, Weweru na Muta. Kuwa na familia yake mwenyewe haikumfanya Wangari kuacha kujiendeleza kimasomo, kwani mwaka 1971 Waangari alipata PhD na inasemeka kwamba alikuwa ni mwanamke wa kwanza kutoka Afrika mashariki na kati kufikia kiwango hicho cha elimu. Na mwaka 1977 alikuwa Profesa.

MWANZO WA KUWA MWANAMAZINGIRA NA KUINGIA KATIKA SIASA.

Mwaka 1974 Bwana Mwangi Mathai muwewe na Waangari aliamua kugombea ubunge katika jimbo la Langata, Wangari akiwa mkewe ilibidi awe bega kwa bega na mumewe katika kampeni. Bwana Mwangi kama ilivyo kawaida ya wanasiasa aliwaahidi mambo mengi wananchi wake ikiwa ni pamoja na kutatua tatizo la ajira. Wangari alisikiliza kwa makini malalamiko ya wananchi na hakuyachukulia mzaha. Kwa bahati nzuri Bwana Mwangi alishinda kiti cha ubunge, na ni hapo Wangari aliona umefika wakati wa kuyatekeleza yale waliyokuwa wakiahidi. Akaamua kuunda kampuni binafsi iliyoitwa ENVIROCARE malengo yake ikiwa ni kutaka kutengeneza ajira kwa wananchi, lakini kwa bahati mbaya kampuni haikuendelea kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha. Wakati huo huo Wangari alikuwa ameshaanza kujihusisha na harakati za ukombozi wa mwanamke na tayari alikuwa mwenyekiti wa baraza la Taifa la wanawake Kenya, akiwa kiongozi katika baraza hilo aliendelea kupata malalamiko juu ya shida wanazozipata wanawake katika maisha yao ya kila siku, kwamba hawana maji, kuni wala chakula chao na cha mifugo yao na huwalazimu kutembea mwendo mrefu ili kuvipata hivyo.

Wangari aliyatizama yale malalamiko na kuona kuwa ni matokeo ya ugonjwa mbaya uliyoikumba Kenya na nchi nyingi za Afrika. Ugonjwa wa kuharibu na kutokujali kabisa mazingira, miti kukatwa ovyo bila kupandwa mingine ndio aligundua kuwa na chanzo shida zote wanazozipata wananchi wa Kenya. Hivyo akaja na wazo la kuanzisha mradi wa kupanda miti kwani miti huilinda ardhi mmomonyoko wa udongo, huifadhi vyanzo vya maji, hutoa chakula, mbao za kujengea, kuni na huweza kuwa chanzo kipato na mambo mengine mengi.

Hivyo tarehe 05/06/1977 ambayo pia ilikuwa ni siku ya mazingira duniani, Wangari alizindua rasmi kampeni ya upandaji miti Kenya, yeye na wenziye walianza kwa kupanda miti saba katika bustani ya Kamukunji Nairobi. Na kuanzia hapo Jumuiya vuguvugu ya ukanda wa kijani ilizaliwa (The Green Belt Movement).

Ingawa jambo hili alilolianzisha Wangari ni jema na lina nia nzuri kwa Wananchi lakini si wote walioliunga mkono. Baada ya kusimama na kuonekana hana mzaha kwa kile anachokifanya hasa akiwa mwanamke, upinzani ulianza kujitokeza kuanzia katika familia yake hadi katika serikali tawala kipindi hicho chini ya Rais Daniel Moi.
Kwa upande wa kifamilia, mumewe bwana Mwangi kama ilivyo kawaida ya wanaume wengi wa kiafrika kutaka kutawala wake zao, hapa ilishindikana kabisa kwani alikuta mkewe ni mtu anayesimama na kupigania kile anachokiamini ni kweli. Matokeo ya haya yote bwana Mwangi aliamua kutoa talaka kwa madai kwamba mkewe ni mkaidi mno, msomi mno mwenye mafanikio makubwa na ni kazi kubwa kumthibiti. Ndoa yake ilivunjika miaka ya themanini.

Kwa upande wa serikali, alipata matatizo kwa vile alikuwa na ujasiri wa kudiriki kuisema serikali ya Moi hadharani bila woga kitu ambacho kilimsababishia kutiwa gerezani mara kadha wa kadha, kupigwa hadi kupoteza fahamu na askari. Lakini katika mambo hayo yote linalokumbukwa zaidi ni lile la miaka ya tisini, ambapo serikali ilitaka kutumia eneo la bustani ya kupumzikia ya Uhuru Park ya Nairobi kujenga jengo la ghorofa 62 ikiambatana na sanamu yake yenye urefu wa futi 60 vyote hivi vikikadiriwa kugharimu dola za kimarekani milioni 200, ambazo nazo ni za kukopwa katika mashirika ya kigeni. Kwa hali moja au nyingine wako ambao hawakulipenda wazo hili lakini kutokana na kukosa ujasiri wa kumkosoa Rais Moi hakuna aliyediriki kupinga. Wangari mwanamke wa shoka alisema hakijengwi kitu hapa. Alikuwa na sababu kuu mbili:
1. Sababu ya kimazingira - kwamba ni kwanini litumike eneo la kupumzikia watu
kujenga ghorofa hilo? ..akaendelea kwamba "Tembo na Vifaru wanatengewa sehemu
za kupumzikia, kwa nini na binadamu wasiwe na sehemu ya kupumzikia?

2. Sababu za kiuchumi - kwamba inakuwaje nchi kama Kenya ambayo watu wake wanakufa
kwa njaa na wakati huo huo inakabiriwa na madeni makubwa, bado inataka kukopa
fedha zote hizo kwa ajili ya jengo moja tu la fahari?.

Msimamo wa Wangari ulifanya mashirika yaliyokuwa yamekubali kutoa fedha hizo kubadili mawazo yao na wazo la kujenga jengo la fahari na sanamu ya Moi kuishia hapo. Kutokana na hili Rais Moi alikasirika sana hadi kuifunga ofisi ya Green belt Movement, ingawa baadaye ilifunguliwa. Na kuanzia hapo alimbatiza jina la 'Mad Woman'. Pamoja na hayo yote bibi Wangari hakukata tamaa kufanya kile alichoamini kuwa anatakiwa kukifanya na hakujua ni kwa kiasi gani kumbe dunia ilikuwa ikimuunga mkono hadi mwaka 2004 ambapo alishangazwa kwa kuchaguliwa kwake kuwa mshindi wa Nishani kubwa ya Amani duniani.

UHUSIANO KATI YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA NA AMANI DUNIANI.

Kama nilivyosema hapo awali kwamba mimi pia sikuelewa uhusiano uliopo kati ya upandaji wa miti na amani duniani, kuna watu wengi ambao pia hili liliwatatiza na kupelekea watu wengi kutaka kujua uhusiano uliopo. Na Bibi Wangari alijibu kama ifuatavyo....
Vita vyote vilivyopo duniani leo ni vita vya kugombea mali asili kama ardhi yenye rutuba, maji, mafuta, madini n.k na watu wamesahau kwamba hivi vyote vinatokana na utunzaji mzuri wa mazingira ambao hupelekea kutokupungua kwa mali asili, na hivyo kila mmoja kupata za kumtosha, hali ambayo inapunguza migogoro ya kunyang'anyana na kufanyiana hila za kuuana. Kwa hiyo basi kwa kupanda miti tu kunaweza kuhakikisha amani kubwa sana duniani, kwani miti italeta mvua, ardhi itapata rutuba, wafugaji hawatatapatapa kutafuta malisho, kuni zitakuwepo za kutosha, chakula cha kutosha, umeme n.k na ni kwa dhana hii pekee ya Bibi Wangari ya kupenda kushughulika na chanzo cha tatizo ndiyo iliyompelekea kupata Nishani ya Amani ya Nobel mwaka 2004. Na kuanzia hapo dunia ilianza kumtafuta ili kupata zaidi busara zake. Miongoni akiwa ni Oprah Winfrey. Hapa pia kuna hotuba yake aliyoitoa mwaka huu katika chuo cha Connecticut kilichopo Marekani, kwa kweli hotuba hii nimeipenda sana na inatia moyo sana hasa kwa wale tunaopenda kusimama katika ukweli wa lile unaloliamini hata kama hakuna anayekuunga mkono.

Mungu mbariki Mama Wangari Muta Maathai.

25 June 2006

Yupi anayepaswa kutolewa bungeni?... anayesinzia kikaoni au aliyevalia??


Hapo majuzi nadhani wote tuliipata hii habari ya mbunge Amina Chifupa kutolewa katika kikao cha bunge kutokana na kofia aliyokuwa amevaa ambayo haikuendana na kifungu kimojawapo cha sheria ya bunge, hivi vifungu vya sheria bado vinanichanganya ina maana kuna vifungu vya sheria vinavyoruhusu kusinzia wakati kikao kikiendelea? nauliza hivi kwa sababu sijawahi kuona mbunge akitolewa kikaoni kwa sababu anasinzia ingawa nusu yao huwa wanasinzia. Hivi ni hadi lini watanzania tutakuwa tukiendelea kukemea mambo mepesi mepesi na kumezea mazito?

Haya habari ya Chifupa hiyo hapo chini kama hukubahatika kuisoma.


Mbunge wa CCM wa Viti Maalum, Mheshimiwa Amina Chifupa leo asubuhi amejikuta akitolewa nje ya ukumbi wa Bunge wakati kikao kikiendelea.

Zali lenyewe lilianza hivi:
Kikao kilianza asubuhi kama kawaida, waheshimiwa wakaingia ndani ya ukumbi na kila mmoja kuketi kwenye siti yake.

Dua iliporomoshwa ya kuliombea Bunge na Taifa, kama kawaida na baadaye kipindi cha maswali na majibu kikaanza.

Hata hivyo ilipotimu kama saa 3:22 hivi, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Samwel Sitta akasema, ’’ Kabla ya kuendelea namuomba Mheshimiwa Amina Chifupa atoke nje akavue kofia yake,’’.

Baada ya sentesi hiyo, Spika alinyamaza kidogo halafu akaendelea, ’’Ni kwa mujibu wa kanuni za Bunge...Mheshimiwa, unaweza kuvua halafu ukarejea tena...siyo moja kwa moja’’.

Mheshimiwa Amina Chifupa alikuwa amevalia kofia ya pama nyeusi inayomechi na nguo zake.

Baada ya tangazo hilo la Spika, Mheshimiwa Amina Chifupa, alisimama na kutoka nje ya ukumbi.

Hata hivyo Spika amefafanua kuwa suti ya Ulaya ikiwa imekamilika ni ruksa kutinga nayo Bungeni.

Akasema kanuni ya 74 kifungu cha tatu ndiyo inayozungumzia mavazi ya kike Bungeni.

Hata hivyo wakati tunakwenda mitamboni mheshimiwa Chifupa alikuwa tayari amerejea ukumbini akiwa hana kofia hiyo.

27 May 2006

Graca Simbine Machel.


Kuna nchi nyingi sana za Afrika ambazo unaweza kuzungumzia historia zake bila kutaja wake wa viongozi waasisi wa mataifa hayo na bado historia ikakamilika. Kwa nchi ya Msumbiji kitu hicho hakipo!. Hauwezi kuelezea historia ya Msumbiji bila kumuhusisha bibi Graca Machel ambaye ni mjane wa Rais wa kwanza wa Msumbiji Ndugu Samora Machel(Mzee wa kombati)

Graca Simbine ni mwanamke mwenye hulka ya upole lakini ni mwenye akili nyingi na makini sana katika utekelezaji wa mambo yake. Ni mtu asiyekurupuka wala kuyumbishwa na mikumbo ya kijamii. Kwa ufupi ni mtu anayefanya jambo kutokana na imani yake inavyomuongoza.

Mwanamke huyu wa shoka alizaliwa tarehe 17-10-1946 katika eneo la pwani ya ukanda wa Gaza nchini Msumbiji. Akiwa ni mtoto wa mwisho kati ya watoto sita wa mzee Simbine na bibi Nelly ni yeye peke yake ambaye hakubahatika kumuona baba yake kwani alizaliwa majuma matatu baada ya baba yake kufariki. Mzee Simbine ambaye alikuwa akifanya kazi katika misheni ya Methodist hapo kijijini, aliacha maagizo kabla ya kufa kwake kwamba mkewe na watoto wake wakubwa ni lazima wahakikishe mdogo wao (Graca) anakwenda shule hadi masomo ya juu. Alipofikisha miaka 6, dada yake mkubwa aliyekuwa mwalimu alimchukua na kumuingiza shule, anasema dada yake alikuwa ni kama mama yake wa pili kwa jinsi alivyomlea vizuri na kuhakikisha anafanya vizuri katika masomo yake, na kutokana na usimamizi mzuri wa dada yake aliweza kufaulu masomo yake ya msingi na kupewa nafasi na misheni ya Methodist kwenda kusoma sekondari. Anasema akiwa sekondari ndipo alipoanza kubaini ubaguzi uliopo kati ya weusi na weupe kwani darasani kwao alikuwa mweusi peke yake kwa hiyo aliona jinsi alivyokuwa akibaguliwa na kutengwa na weupe. Lakini kama nilivyosema hapo awali kwamba yeye si mtu wa kuyumbishwa hilo la kubaguliwa halikumfanya kushindwa kuzingatia masomo yake na mara nyingi anasema jambo moja lilikuwa likimfariji kwamba hata kama alikuwa akibaguliwa lakini alijua Msumbiji ni ya kwake na si yao na wao wako kwake, hivyo alifanya masomo yake vizuri na kufanikiwa kupata tena ufadhili wa kwenda chuo kikuu cha Lisbon Ureno kusomea Lugha hiyo ilikuwa mwaka 1968.

Akiwa Lisbon alikutana na watu wengi wenye fikra mbalimbali za kimapinduzi, akasikia pia habari za FRELIMO chama ambacho kilikuwa kinapigania ukombozi wa Msumbiji. Graca akajiunga kwa siri katika chama cha FRELIMO, lakini haikupita muda mrefu serikali ya kikoloni ikagundua anachokifanya Graca na hivyo ikaandaa adhabu ya kwenda gerezani pindi Graca atakaporejea Msumbiji. Graca kwa kulijua hilo ikabidi asimalize masomo yake na kukimbilia nchini Uswisi. Mwaka 1973 akiwa bado ulaya akaamua kujiweka wazi kama mwanasiasa na mpigania uhuru wa nchi yake na mwaka uliofuata 1974 chama cha FRELIMO kilimrudisha Afrika lakini nchini Tanzania ambapo ilimpatia kazi ya kuwa mkuu wa shule ya sekondari ya FRELIMO iliyokuwa Bagamoyo, shule hii siku hizi hujulikana kama shule ya sekondari ya Kaole. Chama cha FRELIMO kilikuwa na shule nyingi za sekondari katika nchi huru za Afrika nia ikiwa ni kuwapatia elimu wananchi wake huku harakati za ukombozi zikiendelea. Akiwa Tanzania alijifunza pia mafunzo ya kijeshi ya kujilinda na ni katika kipindi hiki ndipo alipoweza kukutana na mzee wa kombati Samora Machel. Graca na Samora walianza kama marafiki wa kawaida lakini baadaye urafiki ukazidi na kuwa wapenzi wakati huo ikiwa ni miaka mitatu tu imepita tangu Samora afiwe na mkewe wa kwanza Josina Machel.

Harakati za FRELIMO ziliendelea vizuri kwani mwaka uliofuatia tarehe 25-06-1975 Msumbiji ilijipatia uhuru wake kutoka wa Wareno, mwaka huo huo Graca alifunga ndoa na Samora machel.

Kutokana na elimu yake na uzoefu wake wa kufundisha, na jinsi alivyoweza kuishika vizuri nafasi ya ukuu wa shule ya FRELIMO Bagamoyo, serikali mpya ya Msumbiji iliona haina sababu kumnyima Graca nafasi ya uwaziri wa elimu na utamaduni. Akiwa wanamke pekee na wa kwanza kushika nafasi hiyo kubwa anasema kwanza alipigwa na butwaa na kutetemeka hakujua kama ataweza kuimudu au la!...alijifungia siku kadhaa chumbani kwake akili na kujiuliza kama akikataa si ataonekana mdhaifu? na je akikubali halafu asiimudu si watasema '..unaona matatizo ya kuwapa nafasi wanawake..!!' Lakini baada ya kujufikiria kwa muda alifuta machozi na kuchukua kazi!! Lengo lake likiwa moja, kuhakikisha watoto wote wa Msumbiji wanakwenda shule. Kwa mafanikio makubwa alibadilisha kabisa hali ya elimu ya Msumbiji kiwango cha watoto kwenda shule kiliongezeka mara dufu kutoka watoto 400,000 aliowakuta alipoishika wizara hadi 1,500,000 ikiwa ni asilimia 72 zaidi.

Haya popote penye maendeleo adui hakosi kujitokeza, mwaka 1976 kikundi kidogo cha wananchi wa Msumbiji wakaunda chama cha kuipinga Frelimo kilichojulikana kama RENAMO. Chama hiki kilikuwa kikifadhiliwa na wazungu kutoka Rhodesia(Zimbambwe), Afrika ya kusini na Marekani. Wazungu hawa waliunda na kufadhili RENAMO ili kuiadhibu Msumbiji kwa kuisaidia makazi wafuasi wa ANC. Kazi ya kikundi hiki cha RENAMO ilikuwa ni kufanya uharibifu katika sehemu zote za maendeleo ambapo FRELIMO ilikuwa ikifanya mfano, ilibomoa mashule na hospitali zilizojengwa na FRELIMO, iliharibu reli na mengine mengi, jambo hili lilimtingisha sana Graca ukizingatia wizara yake nayo ilikuwa ni kati ya tageti za RENAMO. Mwaka 1984 Samora Machel alikubali kusaini mkataba na wafadhili RENAMO wa makubaliano ya kuacha kuifadhili RENAMO na FRELIMO kuacha kuipa msaada wa makazi wafuasi wa ANC. Inasemeka kwamba kwa Samora kusaini mkataba ule ni kama alikuwa akisaini mkataba wa kifo chake, kwani miaka miwili baadaye tarehe 19-10-1986 alifariki katika ajali ya ndege inayosemekana ilipangwa na hao hao wazungu wa Afrika ya kusini. Samora alikuwa akirudi nyumbani kutoka katika mkutano Lusaka Zambia.

Kifo hiki kwa Graca kilikuwa ni pigo kubwa sana. Hakuamini ilikuwa ni ajali ya kawaida alijua na alisema waliomuua mume wangu ndiyo walewale waliomfunga Nelson Mandela. Maneno haya alimuandikia Winnie Mandela wakati wa msiba kwamba "wanadhani kwa kukata miti mirefu zaidi katika msitu watakuwa wameteketeza msitu wote!! ni wale wale waliomuua mume wangu ndiyo waliomfunga mume wako.."

Kwa miaka mitano mfululizo tangu Samora Macheli afariki, Graca alivaa nguo nyeusi peke yake. Na ilipofika mwaka 1989 alistaafu wadhifa wake wa uwaziri na kujishughulisha na shughuli za maendeleo ya jamii hasa hasa watoto. Mungu si Athumani Mola akaona si vyema Graca kuendelea kuishi peke yake hivyo akamtafutia mwenzi mwingine ambaye pia ni shujaa wa Afrika Bwana Nelson Mandela. Mwaka 1998 Graca alifunga pingu za maisha kwa mara ya pili na Mandela ambaye alitengana na mkewe Winnie Mandela mwaka 1992. Winnie anadai iko siku ataongea juu ya mahusiano ya watu hawa wawili.

Graca alibarikiwa kupata watoto 7, ambapo wawili ni wa kuzaa mwenyewe na watano ni wa wake wawili wa kwanza wa Samora. Hadi leo hii Graca ameweka rekodi ya kuolewa mara mbili na marais wawili mashujaa wa nchi tofauti tena katika ndoa zote akiwa ni mke wa tatu.

08 May 2006

Da' Mija na wanawake wa shoka yafunga mwaka!!

Shukrani hoi hoi na vifijo vimuendeee ndugu Ndesanjo Macha popote pale alipo kwani kama si yeye leo hii nisingekuwa naandika haya ninayo yaandika. Ndesanjo ndiye aliyenikurupua huko nilikokuwa na kusisitiza kwamba ni lazima nifungue blogu, nilikwepa kwepa lakini wapi jamaa alikuwa na mimi tu mwishowe nikaona ngoja nikate shauri na leo hii nayaona matunda yake. Sio siri ufahamu wangu sasa umeongezeka-ongezeka.

Labda niwapeni kisa kizima cha Ndesanjo kunibabatiza. Nilikuwa katika harakati zangu mtandaoni mara nikakutana na blogu ya Jikomboe, kuangalia vizuri naona Ndesanjo Macha..nikajiuliza huyu mtu huwa namsikia sikia ngoja nione anafanya nini na humu mtandaoni, basi nikaanza kumfuatilia na kwa kweli makala zake zilinitia nguvu sana nikajisemea peke yangu..'haiwezekani huyu mtu lazima nimjue zaidi'.. basi siku moja nikaona nimtupie kaji-swali ambako kanaonyesha niko kinyume na yeye yaani kama mpinzani wake nione atajibu nini!.. mara nyingi mimi nikiona mtu anafanya vitu vizuri hupenda kujua na anapokoselewa hupokeaje hali hiyo? Wee! nilipata jibu hilo mwenyewe nilitulia bahati mbaya nimesahau hata jibu lenyewe labda kama Ndesanjo unalikumbuka. Basi kuanzia hapo Ndesanjo akajua huyu mtu yuko kinyume na mimi kwa hiyo akawa amekaa mkao tayari tayari, mimi sina hili wala lile siku moja nikatoa maoni katika habari fulani ya "Nimtume nani" nikamwambia labda umetumwa wewe kwani Mungu haangalii mtu fulani ili kumtuma". Sasa hapa nikamchanganya kidogo kwamba huyu Da'Mija yuko upande upi? yuko upande wangu au ananidhihaki?... akanipiga swali Kwani wewe kwako Mungu ni nini au ni kitu gani?? Duh! nikaona haya tena mengine...kaka yangu hapa hakunielewa lakini na mimi sikufanya ajizi nikamuelewesha Mungu ni nini, ni nani kwa jinsi nilivyokuwa nikimuelewa. Baada ya maelezo hayo ndiyo akasema wewe binti ni lazima ufungue blogu yako. Basi nikaona huyu Ndesanjo lazima atakuwa ametumwa na kwangu mimi pia. Hivyo nikafungua blogu yangu. Hadi sasa hivi ingawa sina data kamili, lakini ninaamini huyu bwana ndiyo ameweza kushawishi watu wengi zaidi kufungua blogu zao. Ubarikiwe Ndesanjo, tubarikiwe wanablogu wote.

04 May 2006

Boyz 11 men sasa kiboko!!


Haya tena, ahadi ndio zinazidi kumiminwa na uongozi wa awamu ya nne. Hivi majuzi wakati wa sherehe za mei mosi ambapo kitaifa zilifanyikia Shinyanga Ndugu rais ameahidi kushughulikia suala zima la mishahara, sasa sijui ni ya kweli au la! na ni kwa kiwango gani itaongezwa bado sina hakika.. MtiMkubwa kaniletea hii habari hapa ili wote tushuhudie hizi ahadi. Soma habari yenyewe hapo chini...



2006-05-02 16:53:55
Na Mwandishi Wetu, Jijini

Rais Jakaya Kikwete na Waziri wake Mkuu, Bwana Edward Lowassa, marafiki ambao watoto wa mjini waliwahi kuwaita Boyz ll men, wamewadhihirishia Watanzania kwamba hawana mchezo na wamepania kuboresha hali za Watanzania.

Rais Kikwete alidhihirisha hilo jana wakati anahutubia mamia ya wananchi katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi, Rais Kikwete, sherehe zilizofanyika kitaifa mkoani Shinyanga katika uwanja wa Kambarage.

Katika hali ambayo inaonyesha Rais amepania kutofanya mambo ya danganya toto katika uongezaji wa mishahara na kuboresha maslahi ya watumishi, alitangaza mikakati kadhaa.

Mosi: Alisema ataunda tume itakayotoa hali halisi ya maslahi ya watumishi iliyopo Serikalini na kwenye mashirika ya umma.

Rais alisema tume hiyo pamoja na mambo mengine, itashughulikia uchambuzi wa mishahara na maslahi ya watumishi hao.

Kwa mtaji huo, ’watemi’ Serikalini na katika mashirika ya umma ambao siku zote wanapigania kuongezwa kwa maslahi yao wenyewe, sasa wataumbuka.
Pia madaraja makubwa ya watumishi walionacho na akina pangu pakavu tia mchuzi, yataondoka.

Na kwa upande mwingine, watumishi wasio na nafasi ambao hali zao zimedhoofu kutokana na maslahi duni, watatamba katika uwanja wa haki na usawa.

Rais Kikwete alisema tume hiyo ataitangaza rasmi wiki ijayo na anataka kabla ya mwaka huu kuisha iwe imemaliza kazi hiyo.

Alisema mara baada ya Tume kumaliza kazi na kumpa mapendekezo, hataweka usiku na badala yake atayashughulikia mara moja na kutoa uamuzi juu ya hatua za kuchukua.

Pili: Rais ametaka Mabaraza ya Kisekta ya mishahara ya Kima cha Chini cha mishahara yaundwe mengi ili kushughulikia maslahi ya kundi hilo.

Kwa mtaji huo, kilio cha muda mrefu cha walalahoi huenda kikapungua.
Kwa muda mrefu, wafanyakazi wa kima cha chini wamekuwa wakilalamika kwamba ’wako jangwani’ kutokana na maslahi duni.

Tatu: Rais alisema suala la ajira amelishikia bango na kwamba mikakati inakamilishwa na muda si mrefu Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana italifahamisha Taifa.

Alisema dhamira ya Serikali ni kuongeza ajira kwa Watanzania na kwamba imedhamiria kuweka mazingira mazuri ambayo yatawezesha kukuza ajira nchini ili Watanzania wanufaike na kupunguza dhiki ya maisha.

Nne: Rais pia alizungumzia suala la kuajiriwa kwa wageni katika nafasi ambazo zingeweza kufanywa na Watanzania.

Alisema Serikali itakuwa makini na yenye ukali kwa ajira za aina hiyo.
Kwa kauli hiyo, malalamiko yaliyozagaa kwamba kuna Ma TX feki wanafanya kazi ambazo hata Wabongo ambao hawakwenda shule wanaweza kuzifanya, yatapungua.

Wananchi mbalimbali walioongea na gazeti hili kuhusu hotuba ya Rais walisema serikali ya awamu hii ni kiboko na kama yote yaliyoahidiwa yatatekelezwa, hali za Watanzania zitainuka.

27 April 2006

Eti siku ya mtu kuzaliwa ni ya nani?..mama au mtoto?


Pichani juu ni mimi na kaka yangu na chini ni mzaa chema.

Hapo kipindi cha nyuma nilipata kuzua mjadala na mshairi maarufu wa kikundi cha Parapanda Mgunga mwa Mnyenyelwa juu ya hasa ni nani mwenye haki ya kuiita siku yake, je ni mama au mwana? kwa mujibu wa Mgunga anasema siku ya mtu kuzaliwa ni haki ya mama na kama ni sherehe au pongezi zote anayetakiwa kupewa ni mama. Hili nimelikumbuka leo kwa vile ni siku yangu ya kuzaliwa..., haya wewe unasemaje? ni nani anayetakiwa kupewa pongezi katika siku za kuzaliwa?