22 February 2008

Kazi mpya za Msanii Hendrix Lilanga.





Msanii mchoraji maarufu anayeendeleza kazi za babu yake, Hendrix Lilanga ametuletea kazi zake mpya za kufungua mwaka. Hendrix amefungua pia ukurasa wa kazi zake katika mtandao wa picha wa flickr, mtembelee ujionee mwenyewe mambo yake. Anuani yake ya barua pepe bado ni ileile hendrylilanga@yahoo.com au unaweza kuwasiliana nami kwa maelezo zaidi juu ya kazi zake tumia dadamija@yahoo.com

21 February 2008

Hongera kwa siku ya kuzaliwa 21/02.



Leo mzee Mugabe na mwanangu wanaadhimisha siku zao za kuzaliwa, sasa huwa najiuliza sijui na bibie atakuwa na msimamo kama wa babu?, jibu sipati. Lakini yote maisha cha maana Mungu awazidishie maisha marefu. Happy birthday wooote waliozaliwa siku hii.

20 February 2008

Unawafahamu African Mama's?


Basi kama hauwafahamu au hata kama unawafahamu basi jaribu kuwapitia hapa halafu utaniambia mwenyewe kama si wanawake wa shoka hawa.

Je unataka kuwa wa shoka? Fuatilia vidokezo hapo chini.


Wataalamu wanasema kuwa mtu wa shoka si lelemama, inahitaji nidhamu ya hali ya juu katika uendeshaji wako wa maisha ya kila siku. Kwanza kabisa wanakuambia THINK BIG! Endelea msomaji...


Talent: Our Creator has endowed all of us not just with the ability to
sing, dance or throw a ball, but with intellectual talent. Start
getting in touch with that part of you that is intellectual and
develop that,
and think of careers that will allow you to use that.

Honesty: If you lead a clean and honest life, you don't put skeletons
in the closet. If you put skeletons in the closet, they definitely
will
come back just when you don't want to see them and ruin your life.

Insight: It comes from people who have already gone where you're trying
to go. Learn from their triumphs and their mistakes.

Nice: If you're nice to people, then once they get over the suspicion
of why you're being nice, they will be nice to you.

Knowledge: It makes you into a more valuable person. The more knowledge
you have, the more people need you. It's an interesting
phenomenon,
but when people need you, they pay you, so you'll be okay in
life.

Books: They are the mechanism for obtaining knowledge, as opposed to
television.

In-Depth Learning: Learn for the sake of knowledge and understanding,
rather than for the sake of impressing people or taking
a test.

God: Never get too big for Him.

19 February 2008

Wamama..


Hivi ule usemi usemao mafanikio ya mwanaume kwa kiwango kikubwa huchangiwa na mwanamke, ikiwa na maana mkewe ni wa kweli? na kama ni wa kweli je wake za viongozi nao wanaweza kuwekwa katika kundi la wanawake wa shoka?

Nawauliza wadau swali hili kwa vile nimekuwa nikijiuliza sana kama wake wa viongozi ni wanawake wa shoka au vinginevyo. Tusaidiane jamani.